Jumatatu, 25 Agosti 2014

Kamati za bunge maalumu la katiba, zimeendelea kupitia rasimu ya katiba.

Kamati za bunge maalumu la katiba, zimeendelea kupitia rasimu ya katiba huku baadhi zikiondoa vifungu ikiwemo kinachotakiwa mbunge kuongoza kwa mihula mitatu pekee na kile kinachowapa wananchi mamlaka ya kumuondoa mbunge pale wanapoona hafanyi kazi yake vizuri.
Mwenyekiti wa kamati namba tano, Mh Hamad Rashid amesema rasimu ni nzuri lakini kuna licha ya kuwa rasimu hiyo ilikuwa nzuri, ina baadhi ya mapungufu huku akigusia suala la mfumo wa muungano wa serikali tatu uliotaka bajeti ya jeshi igharamikiwe na nchi wahisani jambo alilosema endapo wananchi wa sehemu moja ya muungano wakilikataa, litasababisha jeshi kufanya mapinduzi na kuleta machafuko.
Kwa upande wake katibu wa bunge maalumu la katiba la katiba, Yahaya Hamad Hamissi, amesema kamati ya uongozi ya bunge hilo imeunda kamati ndogo ya watu 10 ili kushughulikia suala la mahakama ya kadhi na uraia pacha kutokana na vipengele hivyo kuwasumbua sana wajumbe.
Wakati baadhi ya wajumbe wa bunge hilo, taasisi mbalimbali pamoja na baadhi ya wanasiasa wakishauri kuahirishwa kwa bunge hilo hadi baada ya uchaguzi mkuu, baadhi ya wajumbe wameeleza wasiwasi wao juu ufinyu wa muda kwa madai kuwa wanajadilin kwa kulipualipua hali ambayo inaweza kuwafanya wasipate katiba bora.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni